Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ufunuo Ukafunuliwa kwa Bengel

    Katika Ujeremani ujumbe huu ulifundishwa na Bengel, mhubiri wa kiLuther na mwalimu wa Biblia. Wakati alipokuwa akitayarisha mahubiri kutoka kwa Ufunuo 21, nuru ya kuja kwa Kristo mara ya pili ikaangaza katika mafikara yake. Unabii wa Ufunuo ukafunuliwa kwa ufahamu wake. Alipofunikwa kwa ukubwa na utukufu wa mambo yaliyoonyeshwa na nabii, akalazimishwa kuacha fundisho hilo kwa mda. Katika mimbara fundisho hilo likamjia tena kwa nguvu. Tangu wakati ule akajitoa mwenyewe kujifunza mambo ya unabii na kwa upesi akafikia kwa imani kwamba kurudi kwa Kristo kulikuwa karibu. Tarehe ambayo aliyoiweka kama wakati wa kurudi kwa mara ya pili kulikuwa katika miaka michache karibu ya wakati ule ambao Miller alitangaza baadaye.TSHM 174.3

    Maandiko ya Bengel yakaenezwa katika jimbo lake mwenyewe la Wurtemberg na kwa sehemu zingine za Ujeremani. Ujumbe wa kurudi ukasikiwa katika Ujeremani, na kwa wakati uleule ujumbe huo ukavuta uangalifu katika inchi zingine.TSHM 174.4

    Huko Geneve, Gaussen akahubiri ujumbe wa kurudi kwa Yesu. Wakati alipoingia katika kazi ya kuhubiri akaelekea kwa mafundisho ya mashaka. Katika ujana wake akapendezwa na mambo ya unabii. Baada ya kusoma Ancient History [Historia ya zamani] ya Rollin, uangalifu wake ukawa kwa sura ya pili ya Danieli. Akashangazwa na namna unabii ulitimilika kwa uaminifu. Hapa palikuwa na ushuhuda kwa maongozi ya Maandiko. Hakuweza kudumu kutoshelewa na akili za kibinadamu, na katika kujifunza Biblia akaongozwa kwa imani ya hakika.TSHM 174.5

    Akafikia kwa imani kwamba kuja kwa Bwana kulikuwa karibu. Alipovutwa na umuhimu wa ukweli huu, akakusudia kuupeleka mbele ya watu. Lakini imani ya watu wengi kwamba mambo ya unabii wa Danieli hayawezi kufahamika ilikuwa kizuizi kikubwa. Mwishowe akakusudia--kama vile Farel alivyofanya mbele yake katika kuhubiri Genève--kwa kuanza na watoto, kwa njia yao akatumainia kuwa wazazi watavutwa. Akasema, “Nikusanya wasikilizaji watoto; kama kundi linaongezeka kuwa, kubwa, kama likionekana kwamba wanasikiliza, wanapendezwa, wanakuwa na usikizi, kwamba wanafahamu na kueleza fundisho, nina hakika kuwa na kundi la pili karibu, na wao, watu wakubwa wataona kwamba ni faida yao kukaa na kujifunza. Wakati jambo hili linapotendeka, ushindi utapatikana.”TSHM 175.1

    Alipokuwa akisema na watoto, watu wakubwa wakaja kusikiliza. Vyumba vya kanisa lake vikajaa na wasikilizaji, watu wa heshima na wenye elimu, na wageni wa inchi zingine wakazuru Geneve. Kwa hivyo ujumbe ukapelekwa kwa sehemu zingine.TSHM 175.2

    Alipotiwa moyo, Gaussen akatangaza mafundisho yake na matumaini ya kuanzisha mafundisho ya vitabu vya unabii. Baadaye akawa mwalimu katika chuo cha elimu ya tabia na sifa za Mungu na dini, akiendelea kwa siku ya juma pili na kazi yake kama mwalimu wa katikisimu, kusema kwa watoto na kuwafundisha katika Maandiko. Kwa kiti cha mwalimu, kwa njia ya vitabu (chapa) na kama mwalimu wa watoto, yeye kwa miaka mingi alikuwa chombo katika kuita uangalifu wa wengi kwa mambo ya unabii ambayo yalionyesha kwamba kuja kwa Bwana kulikuwa karibu.TSHM 175.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents