Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ufufuo wa Kwanza

    Wale “wanaohesabiwa kuwa wamestahili” kwa ufufuo wa kwanza ni “heri na Watakatifu”. “Juu ya hawa mauti ya pili haina nguvu.” Luka 20:35; Ufunuo 20:6. Lakini wale wasiopata msamaha kwa njia ya toba na imani wanapaswa kupokea “mishahara ya zambi,” azabu “kufwatana na matendo yao,” kuishi katika “mauti ya pili.”TSHM 265.4

    Kwani ni jambo lisilowezekana kwa Mungu kuokoa mwenye zambi katika zambi zake, anamwondolea maisha yake ambayo makosa ilinyanganya na ambaye amejionyesha mwenyewe kwamba hastahili. ” Maana bado kidogo na mwovu hatakuwa; ndiyo utafikiri sana pahali pake, naye hatakuwa,” “Na watakuwa kama hawakuwa mbele.” Zaburi 37:10; Obadia 16. Wanazama katika usahaulifu usiokuwa na matumaini ya milele.TSHM 265.5

    Hivi ndivyo itakavyofanywa mwisho wa zambi. “Umeharibu waovu, Umefuta jina lao kwa milele na milele. Adui wamekoma, wameachwa ukiwa kwa milele.” Zaburi 9:5,6. Yoane katika Ufunuo anasikia wimbo wa furaha wa sifa usiochafuliwa na sauti hata moja ya kutopatana. Hakuna nafsi za watu zinazotukana Mungu wakati wanapojinyonga katika maumivu mabaya isiyokuwa na mwisho kamwe. Hakuna viumbe vya taabu katika jehanum watakaochanganyisha na yawe yao ya nguvu pamoja na nyimbo za waliookolewa.TSHM 266.1

    Juu ya kosa kuhusu maisha ya milele ya asili kunabaki mafundisho ya ufahamu katika mauti. Kulingana na maumivu mabaya ya milele, ni kinyume kwa Maandiko, kwa akili, na kwa mawazo yetu ya kibinadamu.TSHM 266.2

    Kufuatana na imani ya watu wengi, waliokombolewa katika mbingu wanafahamu yote yanayofanyika duniani. Lakini namna gani ingekuwa na furaha kwa wafu kujua mateso ya walio hai, kuwaona wakiendelea na huzuni, uchungu, na maumivu makuu ya maisha? Na ni chukizo la namna gani kuamini ya kama mara pumzi inapotoka mwilini nafsi ya roho isiyotubu inawekwa kwa ndimi za jehanum!TSHM 266.3

    Maandiko yanasema nini? Mtu hana ufahamu katika mauti: “Pumuzi yake inatoka, anarudia udongoni; siku ileile mafikiri yake yanapotea.” “Maana walio hai wanajua ya kwamba watakufa: lakini wafu hawajui kitu, ... Mapendo yao na kuchukia kwao na wivu wao umepotea; wala hawana sehemu tena milele katika neno lo lote linalofanyika chini ya jua.’‘ “Kwa kuwa Hadeze haiwezi kukusifu, wala kufa hakuwezi kukutukuza; wale wenye kushuka kwa shimo hawawezi kutarajia kweli yako. Mwenye uhai, mwenye uhai, ndiye atakayekusifu, kama mimi leo.” “Maana katika mauti hapana ukumbusho juu yako, Katika Hadeze nani atakayekupa asante?” Zaburi 146:4; Muhubiri 9:5,6; Isaya 38:18, 19 ; Zaburi 6:5.TSHM 266.4

    Petro siku ya Pentekote akatangaza ya kwamba Dawidi “alikufa, akazikwa, na kaburi lake ni kwetu hata leo.” “Maana Dawidi hakupanda katika mbingu.” Matendo 2:29,34. Neno ya kwamba Dawidi akingali katika kaburi hata ufufuo linaonyesha kwamba wenye haki hawaende mbinguni wanapokufa.TSHM 266.5

    Akasema Paulo: “Maana kama wafu hawafufuliwi, basi Kristo hakufufuliwa: na kama Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure; mungali katika zambi zenu. Basi wao waliolala katika Kristo wamepotea.” 1 Wakorinto 15:16-18. Kama kwa miaka 4000 wenye haki walikwenda mara moja katika mbingu wakati wa kifo, namna gani Paulo amesema ya kwamba kama hakuna ufufuo, “na wao waliolala katika Kristo wamepotea”?TSHM 266.6

    Wakati alipokuwa karibu kuacha wanafunzi wake, Yesu hakuwambia ya kwamba wangekuja mara moja kwake: “Ninakwenda kuwatengenezea ninyi pahali,” Akasema “Na kama ninakwenda kuwatengenezea ninyi pahali, nitakuja tena, na nitawakaribisha ninyi kwangu.” Yoane 14:2,3. Paulo anatwambia zaidi ya kwamba “Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni, na sauti kubwa, na sauti ya malaika mukubwa, na pamoja na baragumu ya Mungu: Nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza; kisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, kukutana na Bwana katika hewa, na hivi tutakuwa pamoja na Bwana milele. Na anaongeza: “Basi mufarijiane kwa maneno haya.” 1 Tesalonika 4:1618. Katika kuja kwa Bwana, minyororo ya kaburi itavunjika na “wafu katika Kristo” watafufuliwa kwa uzima wa milele.TSHM 267.1

    Wote watahukumiwa kwa kupatana na mambo yaliyoandikwa katika vitabu na kulipwa kama vile matendo yao yalivyokuwa. Hukumu hii haitafanyika katika mauti. “Kwa maana ameweka siku, atakayohukumu dunia kwa haki.” “Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, elfu kumi, ili afanye hukumu juu ya watu wote.” Matendo 17:31; Yuda 15.TSHM 267.2

    Lakini kama wafu wamekwisha kufurahishwa na mbingu ao kujinyonga katika ndimi za moto ya jehanum, ni haja gani ya hukumu ijayo? Neno la Mungu linaweza kufahamika katika mafikara ya kawaida. Lakini ni fikara gani la haki tunaweza kuona wala hekima ao haki katika maelezo inayokubaliwa na wengi? Je, wenye haki watapokea sifa, “Verna, mutumwa mwema na mwaminifu, ... ingia katika furaha ya bwana wako,” wakati walikuwa wakikaa machoni pake kwa miaka mingi? Je, waovu wameitwa kutoka taabuni kupokea hukumu kutoka kwa Mwamzi, “Ondokeni kwangu, ninyi muliolaaniwa, endeni katika moto wa milele”? Matayo 25:21,41.TSHM 267.3

    Maelezo juu ya maisha ya milele ya nafsi ya roho yalikuwa mojawapo ya mafundisho ya uwongo ambayo Roma ilipokea kutoka kwa ushenzi. Luther aliyapanga pamoja na hadisi kubwa (za uwongo) vinavyofanya sehemu ya mtu wa uchafu ya maagizo ya Roma. Biblia inafundisha ya kwamba wafu wanalala hata ufufuo.TSHM 267.4

    Pumziko la heri kwa wenye haki waliochoka! Wakati ukiwa mrefu ao mfupi, lakini ni wakati kwao. Wanalala; wanaamshwa kwa baragumu ya Mungu kwa maisha ya milele ya utukufu. “Kwa sababu baragumu italia, na wafu watafufuliwa wasiwe na kuoza. ... Lakini wakati ule wa kuoza utakapovaa kutokuoza, na ule wa mauti utakapovaa kutokufa, wakati ule litakapotimia neno lililoandikwa; Mauti imemezwa kwa ushindi”. 1 Wakorinto 15:52-54.TSHM 267.5

    Kuitwa kutoka kwa usingizi wao, wanaanza kufikiri ni wapi waliishia. Shituko la mwisho lilikuwa ni maumivu makali ya mauti; wazo la mwisho, kwamba walikuwa wakianguka chini ya uwezo wa kaburi. Wanapofufuka kutoka kaburini, wazo lao la kwanza la furaha, litakaririwa katika shangwe la ushindi: Ee mauti, uchungu wako ni wapi?” 1 Wakorinto 15:55. “Ee kaburi, kushinda kwako ni wapi?TSHM 268.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents