Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Jerome Anapata Toba na Uhodari Mpya

    Upesi akapelekwa tena mbele ya baraza. Waamzi hawakutoshelewa na kujitaa kwake. Ila tu kwa kukataa wazi wazi kwa ukweli ndipo Jerome angaliweza kuokoa maisha yake. Lakini alikusudia kukubali imani yake na kufuata ndugu yake mfia dini kwa miako ya moto.TSHM 46.3

    Alikataa kujikania kwake kwa kwanza na, kama mtu mwenye kufa, akadai kwa heshima apewe bahati ajitetee. Maaskofu wakashikilia kwamba angekubali tu ao kukana mashitaka yaliyoletwa juu yake. Jerome akakataa juu ya udanganyifu kama ule. “Mumenishika bila kusema siku mia tatu na makumi ine katika gereza la kutiisha,” akasema; “Munanileta basi mbele yenu, na kutoa sikio lenu kwa adui zangu za kibinadamu, munakataa kunisikia. ... Mujihazari kuto kufanya zambi juu ya haki. Lakini mimi, niko binadamu zaifu; maisha yangu ni ya maana kidogo; na ninapo waonya si kwa kutoa hukumu isiyo kuwa ya haki, nasema machache kwa ajili yangu mwenyewe kuliko kwa ajili yenu.”TSHM 47.1

    Maombi yake mwishowe yakakubaliwa. Mbele ya waamzi wake, Jerome akapiga magoti na akaomba kwamba Roho ya Mungu ipate kutawala mawazo yake, ili asiweze kusema kitu cho chote kinacho kuwa kinyume cha ukweli ao kisichofaa kwa Bwana wake. Kwake siku ile ahadi ikatimia “Wakati wanapowapeleka ninyi, musisumbuke namna gani ao neno gani mutakalolisema; kwa sababu mutapewa saa ile neno mutakalosema. Kwa maana si ninyi munaosema, lakini Roho ya Baba yenu anayesema ndani yenu.” Matayo 10:19, 20.TSHM 47.2

    Kwa mwaka wote mzima Jerome alikuwa katika gereza, bila kuweza kusoma ao hata kuona. Kwani maneno yake yalitolewa kwa hali ya kuwa na mwangaza sana na uwezo kama kwamba hakusumbuliwa wakati kwa kujifunza. Akaonyesha wasikilizi wake mstari mrefu wa watu watakatifu waliohukumiwa na waamzi wasiohaki. Karibu kila kizazi wale waliokuwa wakitafuta kuinua watu wa wakati wao wakafukuzwa. Kristo mwenyewe alihukumiwa kama mfanya maovu kwa baraza la hukumu lisiyo haki.TSHM 47.3

    Jerome sasa akatangaza toba yake na kutoa ushuhuda kwamba Huss hana kosa na kwamba ni mtakatifu. “Nilimjua tokea utoto wake,” akasema. “Alikuwa mtu bora zaidi, mwenye haki na mtakatifu; alihukumiwa, ijapokuwa hakuwa na kosa ... niko tayari kwa kufa. Sitarudia nyuma mbele ya maumivu mabaya yale yanayotayarishwa kwa ajili yangu na adui zangu na mashahidi wa uongo, ambao siku moja watatoa hesabu ya mambo yao ya ujanja mbele ya Mungu Mkuu, ambaye hakuna kitu kinaweza kudanganya.”TSHM 47.4

    Jerome akaendelea: “Kwa zambi zote nilizozifanya tangu ujana wangu, hakuna moja inayokuwa na uzito sana katika akili yangu, na kuniletea majuto makali, kama ile niliyofanya katika mahali hapa pa kufisha, wakati nilipokubali hukumu mbaya sana iliyofanywa juu ya Wycliffe, na juu ya mfia dini mtakatifu, John Huss, bwana wangu na rafiki yangu. Ndiyo! Ninatubu kutoka moyoni mwangu, na natangaza kwa hofu kuu kwamba nilitetemeka kwa haya sababu ya hofu ya mauti, nililaumu mafundisho yao. Kwa hiyo ni naomba ... Mwenyezi Mungu tafazali unirehemu zambi zangu, na hii kwa upekee, mbaya kuliko zote.”TSHM 47.5

    Kuelekeza kwa waamuzi wake, akasema kwa uhodari, “Muliwahukumu Wycliffe na John Huss ... mambo ambayo walihakikisha, na yasiyo ya udanganyifu, nafikiri, pia vile vile na kutangaza, kama wao.”TSHM 48.1

    Maneno yake yakakatwa. Maaskofu wakitetemeka na hasira, wakapaza sauti: “Haja gani iko pale ya ushuhuda zaidi? Tunaona kwa macho yetu wenyewe wingi wa ukaidi wa wapinga dini!”TSHM 48.2

    Bila kutikiswa na tufani, Jerome akakaza sauti: “Nini basi! munafikiri kwamba naogopa kufa? Mulinishika mwaka mzima katika gereza la kutisha, la kuchukiza kuliko mauti yenyewe. ... Siwezi bali naeleza mshangao wangu kwa ushenzi mkubwa wa namna hii juu ya Mkristo.”TSHM 48.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents