Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Zambi Zilifutiliwa Mbali

    Katika wakati wa taabu, kama watu wa Mungu walikuwa na zambi zisizoungamwa kuonekana mbele yao wanapoteseka na hofu na maumivu makali, wangezamishwa. Kukata tamaa kungaliondoa imani yao, na hawangeweza kumuomba Mungu kwa ajili ya wokovu. Lakini hawakuficha maovu kwa kuyafunua. Zambi zao zimetangulia kwa hukumu na zimefutiliwa mbali, na hawataweza kuzikumbuka.TSHM 302.1

    Bwana anaonyesha katika matendo yake pamoja na yale ya Yakobo ya kwamba kwa ginsi yo yote hawezi kuvumilia uovu. Wote wanaoachilia ao kuficha zambi zao na kuziruhusu kudumu katika vitabu vya mbinguni bila kuziungama na bila kusamehewa watashindwa na Shetani. Zaidi wanapoheshimu nia wanapoishikilia, ni uhakikisho wa ushindi adui waoa. Wale wanaochelewesha matayarisho hawataweza kuyapata wakati wa hatari, wala wakati wo wote unaofuata. Kesi za wote kama wale ni bila tumaini.TSHM 302.2

    Historia ya Yakobo pia ni matumaini ya kwamba Mungu hatatupa wale ambao, waliodanganywa katika zambi, na wamerudi kwake na toba ya kweli. Mungu atatuma malaika kuwafariji wale wanaokuwa katika hatari. Jicho la Bwana ni juu ya watu wake. Ndimi za moto ya tanuru inaonekana karibu kuwateketeza, lakini Mtakasaji atawaleta kama zahabu iliyojaribiwa ao kutakaswa katika moto.TSHM 302.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents