Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mwishowe ikakusudiwa kwamba mahali ambapo

    Kama amri hii ingekazwa “Matengenezo hayangeweza kuenezwa ... ao kuanzishwa kwa misingi ya nguvu ... mahali ambapo ilikwisha kuwako.” Uhuru ungalikatazwa. Mazungumzo hayangaliruhusiwa. Matumaini ya ulimwengu yangeonekana kukomeshwa.TSHM 92.2

    Washiriki wa kundi la injili wakaangaliana kwa hofu: “Kitu gani kinachofaa kufanywa?” “Je, wakuu wa Matengenezo wanapaswa kutii, na kukubali amri hiyo? ... Waongozi wa Luther wakapewa uhuru wa ibada ya dini yao. Fazili ya namna moja ikatolewa kwa wale wote waliokubali Matengenezo kabla ya kuwekwa kwa amri walikuwa wamekwisha kukubali maoni ya matengenezo. Je, jambo hilo halinge wapendeza? ...TSHM 92.3

    “Kwa furaha wakaangalia kanuniambapo matengenezo yaliwekwa kwa msingi ulioazimiwa, na wakatenda kwa imani. Kanuni ile ilikuwa nini? Ilikuwa haki ya Warumi kushurutisha zamiri na kukataza uhuru wa kuuliza swali. Lakini, hawakuwa wao wenyewe na watu wao Waprotestanti kuwa na furaha ya uhuru wa dini? Ndiyo, kama fazili ya upekee iliyofanywa katika mapatano, lakini si kama haki. ... Ukubali wa matengenezo yaliyotakiwa kwamba ruhusa ya kuingia uhuru ya dini ilipashwa kuwa tu kwa mategenezo ya Saxony na kwa pande zingine zote za misiki ya kikristo uhuru wa kuuliza swalina ushuhuda wa imani ya matengenezo vilikua kuasi na vilipashwa kuuzuriwa kifungoni na kifo cha kuchomwa kwa mti. Je, waliweza kuruhusu kutumia mahali maalum kwa uhuru wa dini? . . . Je, Watengenezaji wangeweza kujitetea kwamba walikuwa bila kosa kwa damu ya wale mamia na maelfu ambao katika kufuata kwa mapatano haya, wangetoa maisha yao katika inchi zote za kanisa la Roma?”TSHM 92.4

    “Hebu tukatae amri hii,” wakasema watawala. “Katika mambo ya zamiri uwingi wa watu hawana uwezo.” Kulinda uhuru wa zamiri ni kazi ya taifa, na huu ndiyo mpaka wa mamlaka yake katika mambo ya dini.TSHM 92.5

    Wakatoliki wakakusudia kuvunja kile walichoita “ushupavu hodari (uhodari usio wa kuachia mtu nafasi yoyote).” Wajumbe wa miji iliyokuwa na uhuru waliombwa kutangaza kwamba wangekubali maneno ya mashauri yaliyo kusudiwa. Waliomba muda, lakini kwao hawakukubaliwa. Karibu nusu ya watu walikuwa kwa upande wa Watengenezaji, wakijua kwamba musimamo wao utawapeleka kwa hukumu ijayo na mateso. Mmoja akasema, “Tunapashwa kukana neno la Mungu, ao kuchomwa.”TSHM 92.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents