Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uwongo Mkubwa

    Yule aliyeahidi uzima katika uasi alikuwa mdanganyi mkubwa. Na tangazo la nyoka katika Edeni--“Hakika hamutakufa”--lilikuwa hubiri la kwanza lililohubiriwa daima juu ya kutokufa kwa roho (nafsi). Lakini tangazo hili, la kubaki tu kwa mamlaka ya Shetani, linakaririwa kwa mimbara na kukubaliwa kwa watu wengi kwa upesi kama mbele kwa wazazi wetu wa kwanza. Hukumu ya Mungu, “Nafsi inayofanya zambi itakufa” (Ezekieli 18:20) inafanywa kwa kutaka kuonyesha, Nafsi inayofanya zambi, haitakufa, lakini itaishi milele na milele. Kama mtu angalipewa ruhusa ya uhuru ya kukaribia mti wa uzima, baada ya kuanguka kwake, zambi zingalifanywa kukaa milele. Lakini hakuna hata mtu mmoja wa jamaa ya Adamu aliyeruhusiwa kuonja (kutwaa) tunda linalotoa uzima. Kwa hiyo hapo hakuna mwenye zambi wa kuishi milele.TSHM 261.1

    Baada ya Kuanguka, Shetani akaalika malaika zake kufundisha imani katika kutokufa ya milele kwa asili ya mtu. Akiisha kuingiza watu kukubali kosa hili, ilikuwa ni kuwaongoza kuzania kama mwenye zambi angeishi katika mateso ya milele. Sasa mfalme wa giza anamuonyesha Mungu kuwa sultani mkali mwenye kutaka kisasi, kutangaza ya kama anatumbukiza katika jehanum wote wasiompendeza, ya kama wakati wanapojinyonga katika ndimi za moto wa milele, Muumba wao anawatazama chini na kurizika. Kwa hivi ibilisi mukubwa anavika Mtenda mema kwa mwanadamu tabia zake. Ukali ni tabia ya Shetani. Mungu ni mapendo. Shetani ni adui anayejaribu mtu afanye zambi na baadaye akamwangamiza kama awezavyo. Ni mambo ya kuchukiza upendo, rehema, na haki, mafundisho kwamba wafu waovu wanateseka katika jehanum inayowaka ya milele, kwamba kwa zambi za maisha mafupi ya kidunia wanateseka malipizi makali katika maisha yote ya Mungu!TSHM 261.2

    Ni mahali gani katika Neno la Mungu mafundisho ya namna ile inapatikana? Je, mawazo ya wema wa watu wote yageuzwe kwa ukali waushenzi? Hapana, yale si mafundisho ya Kitabu cha Mungu. “Ninavyoishi, Bwana Mungu anasema, sina furaha kwa kufa kwa mwovu; lakini mwovu aache njia yake apate kuishi; geukeni, geukeni mukaache njia yenu mbaya; kwani kwa sababu gani munataka kufa?” Ezekieli 33:11.TSHM 261.3

    Je, Mungu anapendezwa katika kushuhudia mateso yasiyomalizika? Je, Yeye anapendezwa na maumivu wala mazomeo na kilio cha nguvu cha viumbe vinavyoteseka anavyoshikilia katika ndimi za moto? Je, sauti hizi za kuchukiza ziwe sauti za nyimbo katika sikio la yule ambaye ana Upendo Pasipo Mwisho (Mungu)? Loo, matukano gani ya kutiisha! Utukufu wa Mungu hauongezwe kwa kudumisha zambi kupitiamilele na milele.TSHM 262.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents