Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kutakaswa kwa Pahali Patakatifu

    Kusafishwa katika huduma ya kweli kunapaswa kufanyika kwa damu ya Kristo. “Pasipo kumwanga damu hakuna ondoleo. Ondoleo, ao kuondoa Zambi, ndiyo kazi yenye kutimizwa.”TSHM 200.3

    Lakini inawezekana je, zambi kuambatana na Pahali patakatifu mbinguni? Hii inaweza kujifunzwa kwa kuangalia huduma ya mfano, kwa maana makuhani duniani walitumika “kwa mufano na kivuli cha mambo ya mbinguni.” Waebrania 8:5.TSHM 200.4

    Huduma ya patakatifu pa kidunia ilikuwa na sehemu mbili. Makuhani walikuwa wakihudumia kila siku katika Pahali patakatifu, lakini mara moja kwa mwaka kuhani mkuu alifanya kazi maalumu ya upatanisho katika Pahali patakatifu pa patakatifu, kwa ajili ya kusafishwa kwa Pahali patakatifu. Siku kwa siku mwenye zambi anayetubu alileta sadaka yake na, kuweka mukono wake juu ya kichwa cha kafara, akaungama zambi zake, katika mufano kuzihamisha kutoka kwake mwenyewe hata kwa kafara isiyokuwa na kosa. Nyama basi alichinjwa. “Kwa kuwa uhai wa mwili ni katika damu.” Walawi 17:11. Sheria ya Mungu iliyovunjwa ilidai uhai wa mkosaji. Damu, inayokuwa mufano wa uhai wa mwenye zambi ambaye kosa lake huchukuliwa kwa kafara (mnyama), ilibebwa na kuhani katika Pahali patakatifu na kunyunyizwa mbele ya pazia, nyuma ambapo palikuwa na sheria ambayo mwenye zambi aliyovunja. Kwa ibada hii zambi ikahamishwa katika mfano hata Pahali patakatifu. Mara zingine damu haikupelekwa katika Pahali patakatifu, lakini nyama ikaliwa na makuhani. Ibada mbili hizo zilikuwa mufano wa uhamisho wa zambi kutoka kwa mwenye kutubu hata kwa Pahali patakatifu.TSHM 200.5

    Kwa namna hiyo kazi iliendelea kufanyika muda wa mwaka wote mzima. Zambi za Israeli zilikuwa zikihamishwa kwa Pahali patakatifu, na kazi ya kipekee ikawa ya lazima kwa ajili ya ondoleo lao la zambi.TSHM 201.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents