Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    17 / AHADI ZA KURUDI KWA KRISTO

    Ahadi ya kuja kwa Kristo mara ya pili ili kutimiza kazi kubwa ya ukombozi ni msingi wa Maandiko matakatifu. Tangu Edeni, watoto wa imani wamengojea kuja kwa Yule Aliyeahidiwa kwa kuwaleta tena kwa Paradiso iliyopotea.TSHM 141.1

    Enoki, mtu wa saba katika uzao kutoka kwa wale ambao waliokaa katika Edeni, ambaye kwa karne tatu alitembea pamoja na Mungu, akatangaza, “Angalia, Bwana anakuja na watakatifu wake, elfu kumi, ill afanye hukumu juu ya watu wote,” Yuda 14,15. Yobu katika usiku wa taabu akapaaza sauti, “Lakini ninajua ya kuwa Mkombozi wangu ni hai, Na ya kuwa katika siku za mwisho atasimama juu ya inchi:... pasipo mwili wangu nitamuona Mungu: Na mimi mwenyewe nitamuona. Na macho yangu yatamutazama, wala si mwingine.” Yoba 19:25-27. Washairi (poets) na manabii wa Biblia walieleza sana juu ya kuja kwa Kristo katika maneno yenye mwangaza wa moto. “Mbingu zifurahi, na inchi ishangilie, ... Mbele ya Bwana, kwa maana anakuja; Kwa maana anakuja kuhukumu inchi. Atahukumu ulimwengu kwa haki, na mataifa kwa kweli yake.” Zaburi 96:11-13.TSHM 141.2

    Akasema Isaya: “Katika siku ile itasemwa, Tazama, huyu ndiye Mungu wetu, Tumemungoja, ... Tutashangilia na tutafurahi katika wokovu wake.” Isaya 25:9.TSHM 141.3

    Mwokozi akafariji wanafunzi wake na tumaini ya kuwa atakuja tena: “Katika nyumba ya Baba yangu ni makao mengi ... ninakwenda, kuwatengenezea ninyi makao. Na kama ninakwenda, ... nitakuja tena, na nitawakaribisha ninyi kwangu.” “Mwana wa watu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, halafu ataketi juu ya kiti cha utukufu wake; na mbele yake mataifa yote watakusanyika.” Yoane 14:2,3; Matayo 25:31,32.TSHM 141.4

    Malaika walikariri kwa wanafunzi ahadi ya kurudi kwake; “Huyu Yesu aliyechukuliwa toka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja namna hii sawasawa mulivyomwona akikwenda zake mbinguni.” Matendo 1:11. Na Paulo akashuhudia: “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni, na sauti kubwa, na sauti ya malaika mkubwa, pamoja na baragumu ya Mungu.” 1 Watesalonika 4:16. Akasema nabii wa Patemo: “Tazama, anakuja na mawingu; na kila jicho litamwona.” Ufunuo 1:7.TSHM 141.5

    Halafu desturi ndefu iliyoendelea ya uovu itavunjika: “Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala hata milele na milele.” Ufunuo 11:15. “Na kama shamba linalochipuza vitu vilivyopandwa ndani yake: ndivyo Bwana Mungu ataotesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.” Isaya 61:11.TSHM 141.6

    Halafu ufalme wa amani wa Masiya utaimarishwa “Maana Bwana atafariji Sayuni; atafariji pahali pake pote pa pori; atafanya jangwa lake kuwa kama Edeni, na jangwa lake kama shamba la Bwana.” Isaya 51:3.TSHM 142.1

    Kuja kwa Bwana kumekuwa katika vizazi vyote tumaini la wafuasi wake wa kweli. Kati ya taabu na mateso, “na kuonekana kwa utukufu wa Mungu mkubwa, Mwokozi wetu Yesu Kristo” lilikuwa “tumaini la baraka.” Tito 2:13. Paulo alionyesha kwamba ufufuo utafika wakati wa kurudi kwa Mwokozi, wakati waliokufa katika Kristo * watakapofufuka, na pamoja na wahai kuchukuliwa juu kukutana na Bwana katika mawingu. “Na hivi” akasema, “tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi mufarijiane kwa maneno haya.” 1 Watesalonika 4:17.TSHM 142.2

    Kule Patemo mwanafunzi mpendwa akasikia ahadi, “Ndiyo: ninakuja upesi.” Na jibu lake linasimamia ombi la kanisa. “Amina, kuja Bwana Yesu.” Ufunuo 22:20.TSHM 142.3

    Kati ya gereza, kigingi, mahali wanaponyongwa kwa sheria, pahali watakatifu na wafia dini waliposhuhudia kwa ajili ya kweli, kutoka kwa karne nyingi za usemi wa imani yao na tumaini.” Walipohakikishwa na ufufuo wa Yesu mwenyewe, na baadaye ufufuo wao wenyewe wakati wa kuja kwake, kwa sababu hii, “akasema mmojawapo wa Wakristo hawa,” walizarau mauti, na wakapatikana kuwa juu yake, wa Waldenses walitunzaimani ile ile, Wyccliffe, Luther, Calvin, Knox, Ridley, na Baxter walitazamia kwa imani kurudi kwa Bwana. Ndiyo iliyokuwa tumaini la kanisa la mitume, la “kanisa katika jangwa,” na la Watengenezaji.TSHM 142.4

    Unabii hautabiri tu namna na kusudi la kuja kwa Kristo mara ya pili, bali huonyesha ishara ambazo watu wanapashwa kujua wakati siku ile inapokaribia. “Na kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota.” Luka 21:25. “...jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa nuru yake, na nyota za mbingu zitaanguka, na nguvu zilizo mbinguni zitatikisika. Na wakati ule wataona Mwana wa watu akikuja katika mawingu pamoja na uwezo kubwa na utukufu.” Marko 13:24-26.TSHM 142.5

    Muonyeshaji (nabii) basi anaonyesha mojawapo wa ishara zitakazo tangulia kuja kwa mara ya pili: “... tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la inchi, jua likakuwa jeusi kama gunia la manyoya, na mwezi wote ukakuwa kama damu.” Ufunuo 6:12.TSHM 142.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents