Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Vijana Walifundishwa Kuwa Wajumbe (wa injili)

    Wakristo Wavaudois walijisikia kuwa na madaraka makuu ya kutoa nuru yao iangaze. Kwa uwezo wa Neno la Mungu walitafuta kuvunja utumwa ambao Roma ililazimisha. Wahudumu wa Wavaudois walipaswa kutumika kwa miaka tatu katika shamba la misioni kabla ya kuongoza kanisa nyumbani--chanzo cha kufaa kwa maisha ya mchungaji katika nyakati ambazo roho za watu zinajaribiwa. Vijana waliona mbele yao, si utajiri wa kidunia na sifa, bali taabu na hatari na labda mateso ya wafia dini. Wajumbe walitembea wawili wawili, kama vile Yesu alivyowatuma wanafunzi wake.TSHM 25.3

    Kama wangejulisha ujumbe wao wangeuletea kushindwa. Kila mhuburi alikuwa na ujuzi wa kazi fulani ao ufundi, na wajumbe waliendesha kazi yao chini ya kifuniko cha mwito wa kazi ya dunia , kwa kawaida kama mfanya biashara ao ya mchuuzi. “Walichukua mavazi ya hariri, vitu vilivyofanyizwa kwa zahabu, na vitu vingine, ... na walikaribishwa vizuri kama wafanya biashara mahali wangezarauliwa kama wajumbe (missionnaires)” Walichukua kwa siri nakala za Biblia, nzima ao kipande. Mara kwa mara shauku ya kusoma Neno la Mungu ilipoamushwa, sehemu fulani za Biblia ziliachwa kwa wale waliozihitaji.TSHM 25.4

    Kwa miguu wazi na mavazi machafu na safari ya udongo mzito, wajumbe hawa walipita katika miji mikubwa na kuingia kwa inchi za mbali. Makanisa yakasimamishwa kwa haraka njiani walimopita, na damu ya wafia dini ikashuhudia ukweli. Kwa uficho na ukimya, Neno la Mungu likitukana na kupokelewa kwa furaha ndani ya nyumba na mioyoni mwa watu.TSHM 26.1

    Wavaudois waliamini kwamba mwisho wa vitu vyote haukuwa mbali sana. Walipokuwa wakijifunza Biblia walikuwa wanatia moyo kwa kazi yao ya kujulusha wengine juu ya ukweli Walipata faraja, tumaini, na amani kwa kumwamini Yesu. Namna nuru ilifurahisha mioyo yao, walitamani sana kutawanya nyali zake kwa wale waliokuwa katika giza la makosa la kipapa.TSHM 26.2

    Chini ya uongozi wa Papa na mapadri, wengi walifundishwa kutumainia kazi ao matendo yao mazuri kwa kuokolewa. Walikuwa wakijiangalia wao wenyewe, akili zao zilikuwa zikiishi katika hali yao ya zambi, kutesa moyo na mwili, lakini bila kurijika. Maelfu walipoteza maisha yao katika viumba vya watawa (moines). Kwa mafungo ya mara kwa mara na kutesa mwili, kukesha usiku wa manane, kwa kusujudia mahali pa baridi, mawe ya maji maji, kwa safari ndefu--za kwenda kuzuru Pahali patakatifu--kwa kuogopa ya hasira ya kisasi cha Mungu--wengi waliendelea kuteseka hata kuchoka kukadumisha. Bila nyali moja ya tumaini wakazama ndani ya kaburi.TSHM 26.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents