Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    39 / WAKATI WA TAABU

    “Kwa wakati ule Mikaeli atasimama, Mfalme Mkubwa anayesimama kwa ajili ya wana wa watu wako; na kutakuwa wakati wa taabu, kama usivyokuwa mbele tangu wakati taifa lilipokuwa hata wakati ule: na kwa wakati ule watu wako wataponyeshwa, kila mtu atakayeonekana ameandikwa katika kitabu.” Danieli 12:1.TSHM 299.1

    Wakati ujumbe wa malaika wa tatu unamalizika, watu wa Mungu watakuwa wametimiza kazi yao. Wamepokea, “mvua ya mwisho” na wanajitayarisha kwa saa ya kujaribiwa inayokuwa mbele yao. Jaribu la mwisho limekwisha kuletwa duniani, na wote waliohakikishwa kuwa watiifu (waaminifu) kwa amri za Mungu wamepokea “muhuri wa Mungu aliye hai.” Ndipo Yesu anapomaliza uombezi wake katika Pahali patakatifu kule juu na kusema kwa sauti kuu, “Imefanyika”. “Yeye aliye muzalimu azidi kuwa muzalimu; na mwenye uchafu azidi kuwa mchafu; na mwenye haki azidi kufanya haki; na mtakaifu azidi kutakaswa”: Ufunuo 22:11. Kristo amefanya upatanisho kwa ajili ya watu wake na amefutia mbali zambi zao. “Na ufalme na mamlaka, na ukubwa wa falme chini ya mbingu” (Danieli 7:27) ni karibu kutolewa kwa wariti wa wokovu, na Yesu kutawala kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.TSHM 299.2

    Wakati anapoacha Pahali patakatifu, giza inafunika wakaaji wa dunia. Wenye haki wanapaswa kuishi machoni pa Mungu Mtakatifu pasipo mwombezi. Kizuio juu ya waovu kimeondolewa, na Shetani anakuwa na mamlaka kamili juu ya wasiotubu. Kwa mwisho Roho ya Mungu imeondolewa. Ndipo Shetani anatumbukiza wakaaji wa dunia katika taabu kubwa ya mwisho. Malaika wa Mungu wanaacha kushika kwa kuzuia pepo kali ya tamaa ya wanadamu. Ulimwengu wote utahusika katika maangamizo ya kuogopesha zaidi kuliko yale ambayo yalifika juu ya Yerusalema ya zamani. Hapo kunakuwa majeshi sasa tayari, zinangoja tu ruhusa ya Mungu, kueneza ukiwa po pote.TSHM 299.3

    Wale wanaoheshimu sheria ya Mungu watazaniwa kuwa sababu ya mateso ya kuogopesha na umwangaji wa damu ambavyo vinajaza dunia kwa taabu. Uwezo uliofatana na onyo la mwisho umekasirisha waovu, na Shetani atachochea roho ya uchuki na mateso juu ya wote waliopokea ujumbe.TSHM 299.4

    Wakati kuwako kwa Mungu kuliondolewa kutoka kwa taifa la Wayuda, wakuhani na watu waliendeleya kujizania wenyewe kuwa wateule wa Mungu. Utumishi katika hekalu ilikuwa ikiendelea; siku kwa siku baraka ya Mungu ilikuwa ikitakiwa juu ya watu wenye kosa ya damu ya Mwana wa Mungu. Vivyo hivyo wakati hukumu isiyobadilika ya Pahali patakatifu inapokwisha kutangazwa na mwisho wa ulimwengu ulikuwa wenye kuwekwa milele, wakaaji wa dunia hawataitambua. Kawaida za dini zitakuwa zikiendeleshwa na watu wale ambao Roho ya Mungu imeondolewa; juhudi ya shetani kwa kutimiza nia zake mbaya atachukua mfano wa juhudi ya MunguTSHM 299.5

    Kwa namna Sabato inavyokuwa jambo la upekee la ushindani po pote katika jamii ya Wakristo wote, italazimishwa ya kwamba wachache wanaosimama katika upinzani kwa kanisa na serekali hawapashwi kuvumiliwa, ya kwamba ni bora kwao kuteswa kuliko mataifa yote kutupwa katika fujo. “Inafaa kwetu kayafa akasema mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, na kwa hiyo taifa lote lisiangamie”, Yoane 11:50. Neno hili litaonekana la kutibitisha; amri mwishoni itatolewa juu ya wale wanaotukuza Sabato ya amri ya ine, kuwashitaki na kutoa uhuru kwa watu baada ya wakati fulani kuwaua. Kanisa la Roma kwa wakati wa ulimwengu wa mkufuru wa Kiprotestanti katika ulimwengu wa sasa atafuata njia ileilne. Watu wa zamani na Mungu watatumbukuzwa katika musukosuko hiyo ya taabu inaonyesha kama wakati wa taabu yake yakobo. Yeremia 30:5-7. Usiku wa Yakobo wa uchungu, wakati alipo shindana katika maombi kwa kuokolewa kutoka kwa Esau (Mwanzo 32:24-31) inaonyesha tendo la watu wa Munguwakati wa taabu. Sababu ya udanganyifu uliotumiwa kwa kupatabaraka kutoka kwa baba yakeambayo ilikuwaya Esau, Yakobo alikimbia, alipojulishwajuu ya vitisho vya kifo vilivyofanywa na ndugu yake. Baada ya kukaa miaka nyingi mbali na kwao, akachagua kurudi inchini yake ya asili. Alipofikamipakani akajazwa na hofu kwa habari ya kumkaribia Esau, akahakikisha kuwa nduguye atalipisha kisasi. Tumaini pekee la Yakobo lilikuwa ni rehema za Mungu; ulinzi wake wa kipekee ulipashwa kuwa ni maombi.TSHM 300.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents