Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Wesley Anaepuka Kifo

    Watu wa mvuto wakatumia uwezo wao kinyume chao. Wakuu wengi wa kanisa wakaonyesha uchuki, na milango ya makanisa ikafungwa juu ya imani safi. Padri, akiwalaumu juu ya mimbara, akachochea watu wajinga wa giza na waovu. Mara na mara Wesley akaepuka kifo kwa muujiza wa uhuruma ya Mungu. Wakati ilionekana kwamba hakuna njia ya kuepuka, malaika katika umbo la kibinadamu alikuja upande wake na kundi lilianguka na mtumishi wa Kristo akapita katika usalama kutoka hatarini.TSHM 120.5

    Kwa ajili ya ulinzi wake, mojawapo wa matukio hayo, Wesley akasema: “Ingawa wengi walijaribu kukamata ukosi wa shingo yangu ao mavazi, kuniangusha, hawakuweza kufunga kamwe: ila mmoja tu alishika upindo wa kisibau changu ambacho kikabaki mara mkononi mwake; na upindo mwengine, ndani ya mfuko ambao ulikuwamo noti ya benki, ilipasuka lakini nusu yake. ... Mtu wa nguvu nyuma yangu akanipiga mara nyingi, na fimbo kubwa ya mti wa Ulaya (che ne); ambayo kama angalinipaga mara moja tu kwa upande wa nyuma wa kichwa changu, ingalikuwa ni mwisho wangu. Lakini kila mara, pigo likapotoka, sijui namna gani; kwani sikuweza kwenda kuume wala kushoto.”TSHM 121.1

    Wamethodiste wa siku ile walivumilia kicheko na mateso, mara nyingi mauaji. Kwa nyakati zingine, matangazo kwa watu wote libandikwa, kuita wale waliotaka kuvunja madirisha na kunyanganya katika nyumba za Wamethodiste ili wakusanyike kwa wakati ulitolewa na mahali. Mateso ya desturi yakafanyika juu ya watu ambao kosa moja tu lilikuwa ni kutafuta kugeuza wenye zambi kutoka kwa njia ya uharibifu na kuwaingizisha kwa njia ya utakatifu!TSHM 121.2

    Uharibifu wa kiroho katika Uingereza kabla ya wakati wa Wesley ulikuwa katika hali kubwa matokeo ya mafundisho kwamba Kristo alifuta kanuni ya mema na mabaya na kwamba Wakristo hawakuwa na lazima ya kuishika. Wengine wakasema kwamba ilikuwa si lazima kwa wachungaji kuonya watu kutii amri zake, kwani wale ambao Mungu aliowachagua kwa wokovu “wataongozwa kufuata utawa na wema” wakati wale waliohukumiwa laana ya milele “hawakuwa na uwezo kwa kutii sheria ya Mungu.”TSHM 121.3

    Wengine wakishikilia kwamba “wateule hawawezi kukosa neema ya Mungu wala, kunyanganywa kibali cha Mungu,” walipofikia mwisho kwamba “matendo mabaya wanayotenda si maovu, ... na kwamba, baadaye, hawana na nafasi wala kuungama zambi zao ao kuyaacha kwa njia ya toba.” Kwa hiyo, wakatangaza, hata zambi moja katika zambi mbaya kuliko” zilizozaniwa kwa wote kuwa mvunjo mkubwa zaidi wa amri za Mungu kama si zambi mbele za Mungu “kama ikitendwa na mmojawapo wa wateule.” Hawawezi kufanya kitu cho chote kisicho mpendeza Mungu ao kilichokatazwa na sheria.”TSHM 121.4

    Mafundisho haya mabaya yanakuwa sawa sawa na mafundisho ya mwisho kwamba hakuna sheria ya Mungu inayogeuka kama kipimo cha haki, lakini tabia hiyo ilionyeshwa na chama chenyewe na mara kwa mara ilipaswa kubadirishwa. Mawazo haya yote yalitoka kwake ambaye miongoni mwa wakaaji wasio na kosa wa mbinguni alianza kazi yake kwa kuvunja amri za haki za sheria ya Mungu.TSHM 121.5

    Mafundisho haya mabaya juuya amri za Mungu, zisizogeuka kwa kuimarisha tabia ya watu iliongoza wengi kukataa sheria ya Mungu. Wesley kwa uhodari akapinga mafundisho haya ambayo yaliongoza watu kupinga amri ya Mungu, mafundisho juu ya hali ya kila mtu (Predestination). “Neema ya Mungu inayoleta wokovu imeonekana kwa watu wote.” “Mungu Mwokozi wetu anayetaka watu wote waokolewa na kupata ujuzi wa kweli. Kwani kuna Mungu mmoja, na mupatanishi katikati ya Mungu na watu ni mmoja, yule mtu ni Kristo Yesu, aliyejitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote. ” Kristo “Nuru ya kweli inaangazia nuru kila mtu anayekuja katika ulimwengu.’‘ Tito 2:11; 1 Timoteo 2:3-6; Yoane 1:9. Watu wanaoshindwa kupata wokovu ni wale wanaokataa kwa mapenzi yao zawadi ya uzima.TSHM 122.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents