Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kweli Inatakasa

    Mdanganyi mkubwa anakuwa na wazushi wengi waliofanywa tayari kupendeza onjo mbalimbali ya wale ambao angeharibu. Ni mpango wake kuleta ndani ya kanisa watu wasiofaa, wasiogeuza wale watakaoshawishi mashaka na kutoamini. Wengi wasiokuwa na imani kamili katika Mungu wanakubali kanuni zingine za kweli na wanajifanya kuwa Wakristo, na kwa hivi wanawezeshwa kuingiza kosa kama mafundisho ya maandiko. Shetani anajua kwamba kweli, iliyokubaliwa katika upendo, inatakasa nafsi. Kwa hiyo anatafuta kubadilisha maelezo ya uwongo, mifano, injili ingine. Tangu mwanzo, watumishi wa Mungu wamebishana juu ya waalimu wa uwongo, si kama watu wabaya tu, bali kama wenye kufundisha uwongo wa kufisha kwa nafsi. Elia, Yeremia, Paulo, kwa nguvu walipinga wale waliokuwa wakigeuza watu kutoka kwa Neno la Mungu. Ule uhuru ambao unaangaliarau imani kamili hafifu haikupata nafasi kwa hawa watetezi watakatifu wa kweli.TSHM 254.1

    Maelezo yasiyofahamika vizuri na ya kujiwazia tu juu ya Maandiko na maelezo yenye kupingana katika ulimwengu wa Kristo yanakuwa ni kazi ya adui wetu mkubwa kwa kuchafua akili. Ugomvi na fitina miongoni mwa makanisa vinatokana mara nyingi na kupinganisha Maandiko kwa kuunga mkono maelezo ya kupendeza.TSHM 254.2

    Kwa kusimamia mafundisho ya uwongo, wengine wanashikilia juu ya maneno ya Maandiko wanayotenga kando kwa maneno mengine, kutumia maneno nusu ya fungu kama kuhakikisha msimamo wao, huku sehemu iliyobaki inapoonyesha maana kuwa kinyume kabisa. Kwa werevu wa nyoka wanajiingiza wenyewe nyuma ya maneno ya kutengwa yaliyofasiriwa kufurahisha tamaa za mwili. Wengine wanashikilia juu ya sura na mifano, wanayatafsiri kwa kupendeza mawazo yao, pamoja na heshima kidogo kwa ushuhuda wa Maandiko kama mfasiri wake mwenyewe, halafu kuonyesha mambo ya upumbavu wao kama mafundisho ya Biblia.TSHM 254.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents