Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    31 / PEPO WACHAFU

    Malaika wa Bwana na pepo wachafu wanaonyeshwa wazi katika Maandiko na wanaingia katika historia ya wanadamu. Malaika watakatifu wale “wanaotumikia watakaoriti wokovu” (Waebrania 1:14) wanazaniwa kwa wengi kama pepo za waliokufa. Lakini Maandiko inaonyesha hakika kwamba hawa si pepo inayoachana na mwili wa waliokufa.TSHM 249.1

    Mbele ya kuumbwa kwa mtu, malaika walikuwa wakiishi, kwani wakati misingi ya dunia ilipowekwa, ‘’nyota za asubui waliimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipiga kelele kwa furaha.” Yobu 38:7. Nyuma ya kuanguka kwa mtu, malaika walitumwa kulinda mti wa uzima mbele ya mwanadamu kufa. Malaika wanakuwa wakubwa kwa cheo kuliko watu, kwa kuwa mtu aliumba “chini kidogo kupita malaika “. Zaburi 8:5.TSHM 249.2

    Nabii anasema, “Nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi.” Mbele ya Mufalme wa wafalme wanangojea-“ninyi watumishi wake, munaofanya mapenzi yake,” “mukisikiliza sauti ya neno lake,” “majeshi ya malaika elfu nyingi.” Ufunuo 5:11; Zaburi 103:20,21; Waebrania 12:22. Kama wajumbe wa Mungu wanatoka, kama “kuonekana, kwa kumulika kwa umeme,” mruko wao mwepesi sana. Malaika aliyetokea kwa kaburi la Mwokozi, sura yake “kama umeme,” ikawaletea walinzi kwa ajili ya hofu kutetemeka, na “wakawa kama wafu.” Wakati Saniaribu alipomtukana Mungu na kuogopesha Waisraeli, “malaika wa Bwana alitoka, akapiga katika kambi ya Waasuria watu elfu mia moja makumi mnane na tano.” Ezekieli 1:14; Matayo 28:3,4; 2 Wafalme 19:35.TSHM 249.3

    Malaika wanatumwa kwa kazi ya rehema kwa wana wa Mungu. Kwa Abrahamu, kwa ahadi za baraka; kwa Sodomo, kuokoa Loti kwa maangamizo; kwa Elia, karibu kuangamizwa katika jangwa; kwa Elisa, kwa magari ya farasi ya moto alipofungiwa ndani na adui zake; kwa Danieli, wakati alipoachwa kuwa mawindo ya simba; kwa Petro, alipohukumiwa kifo katika gereza ya Herode; kwa wafungwa kule Filipi; kwa Paulo katika usiku wa zoruba juu ya bahari; kwa kufungua akili ya Kornelio kwa kukubali habari njema; kwa kutuma Petro pamoja na habari njema ya wokovu kwa mgeni wa Kimataifa--kwa hivi malaika watakatifu walitumikia watu wa Mungu.TSHM 249.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents