Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    21 / KUTESWA KWA AJILI YA MWENENDO WA MPUMBAFU AO MJINGA

    William Miller na wasaidizi wake walitafuta kuamsha walimu wa dini kwa tumaini la kweli la kanisa na mahitaji yao ya maarifa makubwa ya kikristo. Walitumika pia kwa kuamsha wasiogeuka kwa toba na mabadiliko. “Hawakujaribu kutubisha watu kwa dini fulani. Walitumika bila uchaguzi w makundi ao dini fulani. ” Akasema Miller, “Nilifikiri kusaidia wote. Niliwaza kwamba Wakristo wote wangefurahi katika kutazamia kuja kwa Kristo, na kwamba wale hawakuweza kuona kama mimi hawangekosa kupenda wale waliopashwa kukubali kwa moyo mafundisho haya, sikuwaza kwamba kungeweza kuwa na lazima ya mikutano ya kuachana... Hesabu kubwa ya wale waliogeuka chini ya kazi zangu walijiunga na makanisa mbalimbali iliyokuwako.”TSHM 180.1

    Lakini kwa sababu waongozi wa dini walipinga juu ya mafundisho ya Adventiste, walikatalia washiriki wao haki ya kuhuzuria kuhubiri juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Wala hata kusema kwa ajili ya tumaini lao katika kanisa. Waaminifu walipenda kanisa zao.TSHM 180.2

    Lakini walipoona haki yao kwa kuchunguza mambo ya unabii unakanwa, waliona kwamba uaminifu kwa Mungu unawakataza kuwatii. Kwa hiyo waliona kwamba walikuwa na haki kujitenga. Wakati wa kipwa cha mwaka 1844 karibu elfu makumi tano wakatoka kwa makanisa.TSHM 180.3

    Katika makanisa mengi, kwa miaka nyingi kuongezeka kulikuwako lakini kwa kidogo kufuatana na matendo ya dunia iloyolingana na upungufu kwa maisha ya kiroho. Lakini kwa mwaka ule kulikuwa ushuhuda wa upunguo mkubwa ndani ya makanisa yote ya inchi. Jambo lilielezwa sana kwa magazeti na mimbarani.TSHM 180.4

    Bwana Barnes, mwandishi wa maelezo na mchungaji wa mojawapo wa makanisa makubwa ya Philadelphia, “akasema kwamba ... Sasa hakuna maamsho, hapana kugeuka, hakuna kuonekana sana kwa maendeleo katika neema katika walimu, na hakuna anayekuja kwa mafundisho yake kwa kuzungumza juu ya wokovu wa roho zao...kunakuwa kuongezeka kwa akili ya kidunia Ni vile inakuwa katika makanisa yote.TSHM 180.5

    Katika mwezi wa Februari wa mwaka ule ule, Mwalimu Finney wa Oberlin College akasema: “Kwa kawaida, makanisa ya Kiprotestanti ya inchi yetu, yanavyoonekana, yalikuwa ao baridi ao adui ya matengenezo yote ya tabia na usafi vya wakati huu ... ubaridi wa kiroho unatawala karibu kote kwa wingi wa kutisha; kwa hiyomagazeti ya dini ya inchi yote yanashuhudia ile. ...Kwa wingi sana washiriki wa kanisa wanatawaliwa na mtindo wakisasa (mode),yanaunga mkono mwovu katika makundi ya anasa, katika michezo, katika furaha. ... Makanisa kwa kawaida yanakuwa kwa huzuniyenye kurudia kwa ushenzi. Yalikwisha kwenda mbali ya Bwana na amekwisha kujiondoa mwenyewe kwao.’‘TSHM 180.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents