Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Maombezi ya Kristo

    Maombezi ya Kristo kwa ajili ya mtu katika Pahali patakatifu kule juu ni lazima kwa mpango wa wokovu kama ilivyokuwa na kifo chake msalabani. Kwa njia ya kifo chake akaanza kazi ile ambayo aliyopandia kwa kuitimiza mbinguni. Kwa imani inatupasa kuingia ndani ya pazia, “pahali alipoingia Yesu kwa ajili yetu.” Waebrania 6:20. Hapo nuru kutoka kwa msalaba imerudushwa. Hapo tunapata mwangaza zaidi juu ya siri za ukombozi.TSHM 237.3

    “Yeye anayefunika zambi zake hatasitawi: Lakini yeye anayezikiri na kuziacha atapata rehema.” Mezali 28:13. Kama wale wanaoachilia (ruhusu) makosa yao wangaliweza kuona namna gani Shetani anavyolaumu Kristo kwa maisha yao, wangeungama zambi zao na kuziacha. Shetani anatumika apate utawala wa moyo wote, na anajua ya kuwa kama mawaa yanafurahiwa, atashinda. Kwa hiyo anatafuta daima kudanganya wafuasi wa Kristo kwa werevu wake wa mauti ambao haiwezekani kwao kuushinda. Lakini Yesu alisema kwa wote wanaoweza kumfuata: “Neema yangu inafaa kwako.” “Nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.” 2 Wakorinto 12:9; Matayo 11:30. Hebu kusiwe watu wo wote kuzania makosa yao kama siyakuponyeka. Mungu atatoa imani na neema kwa kushinda.TSHM 237.4

    Sasa tunaishi katika siku kubwa ya upatanisho. Wakati kuhani mkuu alipokuwa akifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, wote walilazimishwa kuhuzunisha roho zao kwa toba ya zambi. Kwa namna ileile, wote wanaotaka majina yao kudumu katika kitabu cha uzima wanapashwa sasa kuhuzunisha roho zao mbele ya Mungu kwa toba ya kweli. Hapo kunapashwa kuwa na uchunguzi mwingi, wa imani ya moyoni. Roho hafifu iliyopendelewa na wengi inapashwa kuachwa. Hapo kunakuwa vita ya nguvu mbele ya wale wote wanaoshinda mivuto mbaya inayoshindana kwa ajili ya utawala. Kila mtu anapashwa kukutwa pasipo awaa ao kikunjo wala kitu cho chote kama hivi.” Waefeso 5:27.TSHM 237.5

    Kwa wakati huu juu ya vitu vyote vingine inafaa kila nafsi kusikia onyo la upole la Mwokozi: “Tazameni, ombeni, maana hamujui wakati ule.” Marko 13:33.TSHM 238.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents