Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kwa Wakati Uliotajwa

    Kwa wakati uliotajwa--mwisho wa siku 2300 katika 1844--kazi ya uchunguzi ikaanza na kufutiwa mbali kwa zambi. Zambi zisizoungamwa na kuachwa hazitafutwa kutoka vitabu vya ukumbusho. Malaika wa Mungu wakashuhudia kila zambi na kuiandika. Zambi inaweza kukanwa, kufichwa kwa Baba, mama, bibi, watoto, na kwa rafiki; lakini inawekwa wazi mbele ya mbingu. Mungu hadanganywe kwa matendo yanayoonekana. Hafanyi makosa. Watu wanaweza kudanganywa kwa wale wanaochafuka ndani ya moyo, lakini Mungu anasoma maisha ya ndani.TSHM 236.1

    Ni wazo la kutisha namna gani! Mshindi mkubwa kupita duniani hawezi kurudisha ukumbusho wa matendo ya siku hata moja. Matendo yetu, maneno yetu, hata makusudi yetu ya siri, ijapo tukiyasahau, yatatoa ushuhuda wake kwa kuhesabiwa haki wala kuhukumiwa.TSHM 236.2

    Katika hukumu matumizi ya kila kipaji yatachunguzwa. Namna gani tumetumia wakati wetu, kalamu yetu ya wino, sauti yetu, mali yetu, mvuto wetu? Tumefanya nini kwa Kristo katika nafsi ya maskini, wenye kuteswa, yatima, ao mjane? Tumefanya nini na nuru pia na kweli tuliyopewa? Ila tu upendo ulioonyeshwa kwa matendo unaohesabiwa kuwa wa kweli. Upendo peke yake mbele ya Mungu wa mbinguni haufanye tendo lo lote la damani.TSHM 236.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents