Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    41 / DUNIA KATIKA UHARIBIFU

    Wakati sauti ya Mungu inapogeuza utumwa wa watu wake, pale panakuwa na muamko wa kutisha wa wale waliopoteza vyote katika vita kubwa ya maisha. Kupofushwa na madanganyo ya Shetani watajiri wakajisifu wenyewe kwa ukuu wao kwa wale wasiofanikiwa sana. Lakini hawakujali kulisha wenye njaa, kuvika wale waliokuwa unchi, kufanya kwa haki, na kupenda rehema. Sasa wameondolewa vyote vilivyowafanya kuwa wakubwa na wameachwa ukiwa (maskini). Wanatazama kwa hofu juu ya kuangamia kwa sanamu zao. Wameuzisha nafsi zao kwa ajili ya anasa ya dunia na hawakuwa watajiri kwa Mungu. Maisha yao ni ya kushindwa, anasa zao zimegeuka kuwa uchungu. Faida ya maisha yao yote imepotea kwa wakati moja. Watajiri wanalilia kuangamia kwa nyumba zao kubwa, kutawanyika kwa zahabu yao na feza, na hofu ya kwamba wao wenyewe wanapashwa kuangamia pamoja na sanamu zao. Waovu wanaomboleza ya kwamba matokeo ni vile inavyokuwa, lakini hawatubu kwa maovu yao.TSHM 318.1

    Mhubiri aliyefanya ukweli kwa kafara makusudi ya kupata upendeleo wa watu sasa anatambua mvuto wa mafundisho yake. Kila mustari ulioandikwa, kila neno lililotamkwa lililoongoza watu kudumu katika kimbilio la uwongo limetawanya mbegu: na sasa anatazama mavuno. Bwana anasema: “Ole wao wachungaji, wanaoharibu na kutawanya kondoo za malisho yangu! ... Angalieni, nitaleta juu yenu uovu wa matendo yenu”. “kwa uwongo mumehuzunisha moyo wao walio haki, nisiowahuzunisha; nakutia nguvu mikono ya mwovu, hata asigeuke toka njia yake ya uovu, na kuponyeshwa hai”. Yeremia 23:1,2; Ezekieli 13:22.TSHM 318.2

    Wahubiri na watu wanaona ya kuwa wameasi juu ya Muumba wa sheria yote ya haki. Kuweka pembeni maagizo ya Mungu kulitoa mwinuko kwa maelfu ya nguvu za uovu, hata dunia ikawa mfereji moja mkubwa wa zambi. Hakuna lugha inayoweza kueleza tamaa ya wasiowaaminifu wanapotazama wale walivyopoteza milele--uzima wa milele.TSHM 318.3

    Watu wanashitakiana wao kwa wao kwa ajili ya kuwaongoza kwa uharibifu, lakini wote wanaunganika kwa kukusanya hukumu yao ya uchungu mkubwa juu ya wachungaji wasiokuwa waaminifu waliotabiri “maneno ya laini” (Isaya 30:10), walioongoza wasikilizaji wao kufanya ukiwa sheria ya Mungu na kutesa wale wangeishika kama takatifu. “Tumepotea”! wameomboleza, “na ninyi ndio munaokuwa sababu yenyewe”. Mikono iliyowatawaza zamani kwa heshima itanyanyuliwa kwa ajili ya uharibifu wao. Po pote kunakuwa vita na umwangaji wa damu.TSHM 318.4

    Mwana wa Mungu na wajumbe wa mbinguni wamekuwa katika vita pamoja na muovu, kwa kuonya, kuangazia, na kuokoa wana wa watu. Sasa wote wamefanya mipango (makusudi) yao; waovu wameungana kabisa na Shetani katika vita kupigana na Mungu. Mabishano si ya Shetani peke yake, lakini pamoja na watu. “Bwana ana mashindano na mataifa”. Yeremia 25:31.TSHM 319.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents