Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tumaini la Vizazi Vyote

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    1 — Kristo Kabla Hajaja Duniani

    Milele hata milele Yesu Kristo yuko katika umoja na Baba. Alikuwa sura ya Mungu, nuru ya upendo wa Mungu, ing’aayo mng’aro wa utukufu wake. Ili kuufunua upendo na utukufu wa Mungu, alikuja katika ulimwengu wetu wa giza. Kwa hiyo Ulitabiriwa kwamba, “Nao watamwita jina lake Immanuel, . . . yaani Mungu pamoja nasi.” Mat. 1:23; Isaya 7:14.TVV 9.1

    Yesu alikuwa “Neno la Mungu” Mawazo ya Mungu yalisikika ndani yake. Ufunuo huu haukutolewa kwa wanadamu waliozaliwa katika dunia tu. Dunia yetu ndogo ndicho kitabu kidogo cha kusomwa na walimwengu. Waliokombolewa na wale wa dunia ambazo hazikuanguka watauona msalaba wa Kristo ambao ndio elimu yao na wimbo wao. Wataona kuwa utukufu ung’aao katika uso wa Yesu ni utukufu wa kujitoa kwake binafsi kwa upendo. Wataona kuwa kanuni ya mbinguni na ya duniani ni upendo wa kujitoa nafsi. Upendo huo “usiojitafutia mambo yake” hutokana na Mungu nao umedhihirishwa kwa njia ya Yesu, ambaye ni mpole na mnyenyekevu.TVV 9.2

    Mwanzo Kristo aliuweka msingi wa dunia. Mkono wake uliiweka dunia katika anga na kuyaweka maua katika nchi. Aliijaza nchi na uzuri, na anga na wingi wa nyimbo. Zaburi 65:6; 95:5. Juu ya vitu vyote aliandika upendo wa Baba.TVV 9.3

    Sasa dhambi imechafua kazi safi ya Mungu, hata hivyo maandiko hayo ya upendo wa Mungu yanadumu kuwako. Hakuna kitu cha ubinafsi kilichoko isipokuwa moyo wa binadamu ndiyo umejazwa na ubinafsi. Kila mti na kichaka na jani hutoa, vitu vya asili vya uhai ambavyo bila hivyo mwanadamu au mnyama hawezi kuishi, na mwanadamu na mnyama huhudumia miti na vichaka na majani.TVV 9.4

    Bahari hupokea maji katika vijito toka nchi, lakini hupata maji hayo ili kutoa. Mvuke unaopanda kutoka baharini huinyoshea nchi na kuiburudisha, ili iweze kutoa machipukizi. Malaika walioko kwenye utukufu furaha yao ni kutoa. Huleta nuru kutoka juu na kuwasaidia wanadamu wapate kumfuata Kristo.TVV 9.5

    Lakini tukiacha hayo yote, tunamwona Mungu ndani ya Yesu. Tunaona kuwa utukufu wa Mungu kutoa. “Siutafuti utukufu wangu wenyewe, ila utukufu wake aliyenituma” Maneno hayo aliyasema Yesu. Yohana 8:50; 7:18. Kristo alipokea kutoka kwa Mungu ili apate kutoa. Kwa njia ya Mwana, maisha ya Baba huwafurikia wote. Kwa njia ya Mwana huduma ya upendo hufurika kwa wote, hivyo kwa njia ya Kristo mzunguko wa manufaa ya Kristo hukamilika.TVV 10.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents